2 684
مشترکین
-824 ساعت
-327 روز
-8430 روز
آرشیو پست ها
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Kansela wa Ujerumani, Friedrich Merz, ameungana na viongozi wa serikali, viongozi wa dini na mamia ya wananchi katika shughuli za kuwaenzi wahanga wa shambulio lililotokea wakati wa maadhimisho ya kila mwaka ya Berlin Pride, mkusanyiko unaotetea haki za jamii ya wapenzi wa jinsia moja unaofanyika jijini Berlin, Ujerumani. Merz aliweka shada la maua katika eneo la kumbukumbu lililoandaliwa kwa heshima ya mwathirika aliyepoteza maisha, huku akitoa wito wa mshikamano wa kitaifa na kusisitiza kuwa Ujerumani haitaruhusu chuki, vurugu na misimamo mikali kuvuruga maadili ya uhuru, usawa na demokrasia. #Kurunzi 27.06.2026
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Iran imesema bado inashikilia udhibiti wa mlango bahari wa Hormuz na haijaomba kurejea kwa mazungumzo ya amani na Marekani.
Kauli ya Tehran inakuja katika wakati ambapo Marekani inadai rais Trump ameamuwa kusitisha vita ili kutoa nafasi kwa mazungumzo, japo vyombo vingi vya habari vya Marekani vimeripoti kwamba hatua ya Trump imetokana na ushauri aliyopewa na jeshi la nchi hiyo.
Mpaka sasa kuna hali ya utulivu mashariki ya kati baada ya Marekani kusitisha vita lakini ripoti zinasema kwamba huenda Iran imeonesha kutikisa kibiriti ili kuusikia mlio wake,ikimaanisha kwamba nchi hiyo huenda imeonesha dalili za kutaka kuujaribu utulivu uliopo ikidaiwa kufanya mashambulizi kadhaa.
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Rais wa Urusi Vladimir Putin amesema ana imani kwamba nchi yake itafanikisha malengo yake katika vita dhidi ya Ukraine. Hata hivyo, ameonya kuwa uchumi wa Urusi unakabiliwa na changamoto zinazohitaji kushughulikiwa ili kuhakikisha ukuaji endelevu na kudumisha uthabiti wa taifa. Putin ameyasema hayo wakati alipokutana na wabunge wanaomaliza muda wao wa kuhudumu katika Bunge la Urusi. #Kurunzi 27.07.2026
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Tizama Ufaransa ikipambana na hali mbili tofauti. Kusini magharibi ni moto wa nyika unaosambaa kwa kasi lakini katikati mwa taifa hilo ni mvua ya mawe iliyotatiza shughuli za usafiri.
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz ameahidi kuchukua hatua za kisiasa baada ya shambulizi lililoua mtu mmoja na kuwajeruhi wengine 29 karibu na maadhimisho ya wapenzi wa jinsia moja mjini Berlin. Kansela Friedrich Merz amesema kutoa matamko pekee hakutoshi, na serikali yake italazimika kujibu kwa utulivu lakini pia kwa uthabiti. Swali kuu kwa Kansela ni jinsi mshukiwa wa shambulio hilo Abdul B, aliyekuwa anafahamika kwa vyombo vya usalama, alivyoweza kufika karibu na maadhimisho ya Christopher Street Day bila kugunduliwa na kutekeleza shambulizi hilo.
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Watu 30 wameuawa katika shambulio katika jimbo la Kaduna, Nigeria https://rfi.my/Cupx.x
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Moto wa nyikani: Rais Macron aiitisha kikao cha dharura cha baraza la Mawaziri https://rfi.my/Cupk.x
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
#HABARI Madereva wa magari ya masafa marefu wameeleza kutoridhishwa na utaratibu unaowalazimu kurejea darasani kila wanapohitaji kuhuisha leseni zao za udereva, wakidai kuwa mafunzo hayo yanajirudia na yanapoteza muda ambao ungeweza kutumika katika shughuli zao za usafirishaji.
Wamesema utaratibu huo unaathiri uzalishaji wao pamoja na shughuli za waajiri, hivyo wamezitaka mamlaka husika kutafuta njia mbadala zitakazorahisisha mchakato wa uhuishaji wa leseni bila kuathiri utendaji wa madereva.
#EastAfricaTv #TogetherTunawakilisha
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Burkina Faso imesema imeingiza dhahabu yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni 6 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2026, baada ya zaidi ya tani 55 kupita kwenye mfumo rasmi.
-
Serikali ya Kapteni Ibrahim Traoré inasema hatua hiyo imeimarisha nafasi ya nchi hiyo kuwa miongoni mwa wazalishaji wakubwa wa dhahabu barani Afrika, ikishika nafasi ya tano.
-
Hata hivyo, wataalamu wanaeleza kuwa kuongeza udhibiti wa serikali kwenye rasilimali kunaweza kuleta faida pamoja na changamoto.
-
Mwandishi wa BBC @frankmavura anasimulia zaidi.
-
-
-
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Maegesho ya magari yajaa maji ya mafuriko, magari yazama
-
Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha huko Vapi, kusini mwa Gujarat nchini India, zimesababisha mafuriko makubwa ambapo maegesho ya magari yalijaa maji na magari kadhaa kusombwa na mafuriko.
-
Maji pia yaliingia kwenye nyumba na maduka, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo.
-
-
-
2 684
+3
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Timu ya taifa ya Tanzania ya wanawake Twiga Stars wataanza kutupa karata yao ya kwanza leo hii katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika kwa wanawake (Wafcon 2026) kwa kucheza na Afrika Kusini (Banyana Banyana)
Michuano ya Wafcon inafanyika nchini Morroco na mchezo huu utachezwa saa 8.00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki
-
-
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Je, mavazi yanaweza kumgharimu mtu kazi?
Hilo ndilo lililomtokea kwa gavana mmoja nchini Uturuki, ambaye ameondolewa madarakani baada ya kuonekana akiwa amevaa nguo za kubana za waendesha baiskeli.
Hata hivyo, uamuzi huo umeibua mjadala mkali. Mwandishi wa BBC @beldeen__waliaula anafafanua zaidi.
-
-
2 684
+5
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Maandamano ya Gen Z India, Nini Kinafuata?
-
Kujiuzulu kwa waziri wa elimu ni jambo lisilo la kawaida kwa serikali ya Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi.
-
Tukio hili limewapa matumaini vijana wengi waliokuwa wakiandamana kwamba sauti zao zinaweza kusikilizwa na kuleta mabadiliko.
-
Pangusa kshoto kufahamu zaidi
-
-
-
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
Profesa Mkenda: Wanafunzi 1,050 kunufaika na Samia Scholarship ndani na nje ya nchi 2026/2027
2 684
️️➟ @HabariTz ✰✰✰
RDC: HRW yaalani uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na kampuni za mafuta https://rfi.my/CupP.x
